... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Kumuunga Mkono Mwingine

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Waebrania 10:24,25 Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Listen to the radio broadcast of

Kumuunga Mkono Mwingine


Download audio file

Si rahisi kumuona mtu anayeonea watu wengine akielekea pabaya ukamuonya au kumsaidia.

Tuligusia kidogo swala hili jana, kwamba ni Mungu tu awezaye kubadililsha moyo wa mwanadamu.Tunaweza kushindana na watu kwa maneno mpaka tunachoka, lakini karibu mara zote, ukaidi wao na kiburi chao vinawazuia wasipokee ushauri wetu mzuri. 

Lakini kuna kitu kingine kinasababisha wasipokee ushauri mzuri.  Ni kikwazo ambacho sisi wenyewe tunakiweka mbele yao. Ebu fikiria kidogo.  Ni mara ngapi ukosoaji mkali wa mtu mwingine umekushitua?  Yaani ni kama wanakuvamia wakijiona kwamba wao ndio wanaojua … hayo yote hayawezi kuleta matokeo mazuri.  Lakini kuna njia mbadala: 

Waebrania 10:24,25  Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia. 

Kuhimizana katika upendo na kazi nzuri, ni jambo, Je!  Wewe binafsi, unapenda kutiwa moyo?  Mimi ninapenda.  Sisi sote tunafurahi tunapotiwa moyo, Yule bwana anajiendea pasipofaa, ni “mkorofi”. Hata kama tungependa kumpiga makofi mtu mkorofi bado hata yeye aliumbwa kwa sura ya Mungu akiwa na vipawa na vipaji ambavyo laiti vingeelekezwa pazuri, angeweza kuonyesha upendo na kutenda mema. 

Endelea kumjali.  Asikukatishe tamaa.  Inatubidi kuendelea kutiana moyo.  

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.