... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Changamoto ya Kuthibiti Mambo

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

1 Petro 4:7,8 Lakini mwishowa mambo yote umekaribia; basi, iweninaakili, mkeshekatikasala. Zaidi ya yote iweninajuhudinyingikatikakupendana; kwasababuupendanohusitiriwingiwadhambi.

Listen to the radio broadcast of

Changamoto ya Kuthibiti Mambo


Download audio file

Njia bora ya kuhakikisha kwamba mambo yaende kama unavyotaka wewe, hata kama ni mambo ya namna gani, ni kuyathibiti.  Hii ingekuwa jibu. Kuthibiti kila kitu lakini maisha hayako hivyo.

Yaani, maisha yana tabia ya kushtuana kumletea mtu mambo yasiyotazamiwa.  Kuna wakati ni mambo ambayo mtu anaweza kukabiliana nayo.  Mara nyingine ni mazito mno.  Wewe umeshayaona, hata mimi … na bila shaka yataendelea kuonekana.  Mara nyingi lakini, tunakumbana nayo vibaya. 

Kuna mara tunajitenga na watu na kujionea huruma peke yetu.  Kuna wakati tunataka kupigana, jambo ambalo haliwezi kusaidia hata kidogo. 

Mtume Petro alikuwaa nawaandikia Wakristo ambao walikuwa wameteswa sana sana!  Wengine wao walikuwa wamechomwa moto wakiwa bado hai.  Yaani nihali inayotisha mno. 

1 Petro 4:7,8 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iwenina akili, mkeshe katika sala.  Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwasababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

Sasa, ni mwitikio upi Mungu anataka tuwenao wakati maisha yanaenda kombo kabisa?  Anataka tujithibiti na kutumia busara kwa kukesha!

Kwa upande mmoja, haitakiwi mtu anune tu na kuanza kuji hurumia.  Lakini kwa upandewa pili, haitakiwi awe na hasira na kutaka kupigana na kulaumu wengine kwa ajili ya matatizo aliyo nayo, akiwafokea na kuwaadhibu.  Kinachotakiwa nikuendelea kupenda watu hata wakati mtu anajaribiwa atende visivyo. 

Kwa hiyo wakati huwezi kuthibiti yanayotokea katika maisha yako, jipe changamoto hii katika Kristo na kwakupitia uwezo wake, uwezo wa Roho Mtakatifu, kujithibiti na kulinda jinsi unavyokabiliana nayo. 

Iweni na akili, mkeshe.

Hili ndilo Neno la Mungu safina lenye afya kwa ajili yako leo.