... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Si Maisha ya Starehe

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Mathayo 4:23,24 Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udahifu wa kila namna katika watu. Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa hawawezi, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya.

Listen to the radio broadcast of

Si Maisha ya Starehe


Download audio file

Kama umewahi kusoma kwenye vitabu vya Injili habari ya huduma ya Yesu ni habari zinazosisimua. Kuponya, kufukuza mapepo, umati wa watu, mahubiri ya ajabu.  Yaani ni mambo makuu.  Lakini kuna mengine hapo si dhahiri.

Ni kweli, ni habari zinazosisimua, uweza wa Mungu ulimkalia Mtu huyu, Yesu Mwana wa Mungu, ni lazima achochee mambo kabisa. 

Mathayo 4:23,24  Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udahifu wa kila namna katika watu.  Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa hawawezi, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya. 

Hata leo tunaweza kuona ule wa kimiujiza ukidhihirika.  Lakini kuna hatari kama tunafuata miujiza, mambo makuu yanayosisimua na maonyesho.   

Lakini chunguza kwanza huduma ya hadhara ya Yesu.  Yeye na wanafunzi wake walitembea kwa miguu maili mingi – kwenye jua kali, kunyeshewa na mvua, joto, baridi, kupanda milima na kushuka mabonde.  Kuna wakati walipata pa kulala na kuna wakati walikosa.

C.S. Lewis alieleza hivi:  Sikutafuta imani ya dini ili nipate “furaha” kwa kuwa nilijua kwamba chupa ya divai ingenipa “furaha” ya namna hiyo.  Kama unataka imani ikupe starehe, nisingekuelekeza kwa Ukristo. 

Usitazamie safari yako ya kumfuata Yesu kwamba itakuwa rahisi. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.